Tuesday 1 November 2016

Habari za wakati huu wapenzi wasomaji wetu,Leo ningependa kutoa mawazo yangu kuhusu suala la kilimo nchini.
Tanzania ni nchi maskini,uchumi wa nchi hii unategemea zaidi kilimo.Kilimo huchangia asilimia 50 ya pato la ndani la nchi hii.Kumekua na jitihada mbalimbali za kuendeleza sekta hii ya kilimo nchini ikiwemo sera iliyo sikika sana ya "KILIMO KWANZA" .Jitihadi hizi zimeweza kufanikiwa kwa kiasi fulani ila kwa kiasi fulani bado uzalishaji wa malighafi nchi bado ni mdogo.
Baada ya kuhudhuria semina mbalimbali nilishangazwa kusikia hadi kuku tunaagiza kutoka nchi za jirani kama Malawi na Kenya.Ni aibu kubwa kwa taifa kama hili lenye ardhi kubwa na rasilimali watu.


VIFARANGA ZAIDI YA 5000 WALIOKAMATWA AIRPORT WAKIINGIZWA NCHINI KWA NJIA HARAMU

Nadhani ni wakati serikali ijaribu kutumia vijana wahitimu katika vyuo mbali mbali katika kuendeleza suala la kilimo nchini. Sera ya  KILIMO KWANZA ilikua na nia nzuri lakini imeonekana kama ilikua na nguvu ya soda,na pia ingelenga vijana moja moja ili kupunguza tatizo la ajira.
Pia vijana waelimishwe kuhusu kilimo,ufugaji na uvuvi ili waweze kujiajiri katika sekta hiyo.Nadhani iwepo sera kwaajili ya kuwahimiza vijana kuhusu kilimo na pia wapewe elimu na mikopo ili waweze kuingia katika uzalishaji malighafi kwa sababu tanzania ya viwanda inakuja hivyo vijana tuwe na Tanzania ya KILIMO ili tuweze kwenda sawa na kasi ya ukuaji wa teknolojia katika viwanda kwani viwanda vitahitaji malighafi hivyo si vyema kuagiza malighafi hizo nje ya nchini wakati nchi ina nguvu kazi na ardhi ya kutosha. Vijana turudi mashambani Tanzania ya tuijenge.

"VIJANA NA TANZANIA YA KILIMO"

KILIMO CHA CHIKICHI NA UTAJIRI KWA MKULIMA

KILIMO CHA UFUTA

UFUGAJI KUKU WA KIENYEJI NA MASOKO YAKE

Thursday 27 October 2016

Habari za wakati huu wapendwa wasomaji wetu na wafugaji,leo ningependa kuwaalika kujifunza kitu kidogo kuhusu kuku chotara na tofauti yake na kuku 100% asilia.
 Kuku chotara hutaga mayai mengi zaidi kulinganisha na kuku 100% asili.kuku chotara hutaga mayai 220-280 kwa mwaka kulingana na ubora wa chakula na mfumo mzima wa ufugaji.



Tetea wa chotara hula kiasi cha 6.8kg kwa muda wa miezi mitano na kuweza kufikia uzito wa 1.8kg kwa kipindi hicho.

Jogoo chotara huweza hula kiasi cha 6.8kg kwa muda wa miezi mitano na kuweza kufikia uzito wa 2.6 kwa muda huo.

Matetea chotara huanza kutaga ndani ya muda wa miezi mitano mpaka sita kutegemea na utunzaji na vyakula wanavyopewe.

Ili kuku hawa watage sana wanatakiwa kula angalau 122g kwa siku za chakula kizuri ili kuweza kutaga kwa muda mrefu.
Kuku hawa wataanza tabia ya kudonoana kama wasipopewa chakula kizuri na chenye virutubisho vya kutosha pamoja na madini.Kuku hawa hudonoana sana na wakati mwingine hupelekea vifo na vidonda


Wednesday 26 October 2016

Magonjwa ya kuku kwa ujumla yapo mengi sana na kuna baadhi ya magonjwa ambayo hayapo hapa nchini,ni vyema kujua dalili hizi za magonjwa mapema ili kuepusha hasara inayoweza kutokea kutokana na vifo ambavyo huchangiwa na magonjwa haya.
Dalili hizo kwa ujumla ni kama ifuatavyo
1.Kuku kupoteza hamu ya kula

2.Kuku kuzubaa na kukaa sehemu moja kwa muda mrefu
3.Kushuka kwa kiwango cha utagaji
4.Vifaranga kudumaa
5.Macho kua mekundu
6.Kujikunja shingo
7.Kutetemeka,kutoa maji maji puani,mdomoni na machoni
      8.Kutoa kinyesi chenye rangi ya kijani,au kinyesi kilicho changanyika na damu au cheupe.
9.  Kukohoa
10.  Kukonda sana

Endapo kuku wako ataonesha mojawapo ya dalili hizo basi mfugaji itamlazimu kutafta daktari wa mifugo au  kuku wapatiwe dawa.kujua madawa mbali mbali ya tazama post nyingine katika blog hii.Pia unaweza kufatilia mambo mbalimbali kuhusu kuku kupitia ukurasa wetu wa INSTAGRAM kwa jina la kukutajiri.

Kuku chotara/kienyeji hufungwa kwa matumizi ya kutaga mayai na pia kwa nyama.Mfugaji atachagua aina na mfumo wa chakula kutokana na yeye anafuga kuku hawa kwa matumizi gani.

Ili kuku wafugwe kwaajili ya mayai fuata ratiba hii ya chakula

Chick starter kwa muda wa miezi miwili(2)
Grower Mash kwa muda wa miezi miwili na nusu(2.5)
Layers mwezi mmoja na kuendelea.

Ili kuku wafugwe kwaajili ya nyama fuata ratiba hii ya chakula

Broiler starter-mwezi mmoja(1)
Grower Mash-Mwezi mmoja(1) 
Broiler Finisher-Mwezi mmoja(1)


Ili kuku wafugwe na kutaga mayai kwaajili kutotolesha fuata ratiba hii ya chakula

Chick Starter-miezi miwili(2)
Grower mash-miezi miwili na nusu(2.5)
Breeders mash-mwezi mmoja na kuendelea.hakikisha majogoo wanapunguzwa na kubaki na uwiano wa jogoo mmoja kwa matetea kumi(1:10)







Ratiba hii ni kwa ufugaji wa kibiashara lakin mfugaji anaweza kuwafuga kuku hawa kwa mfumo wa nusu huria yaani kuku akaachiwa ajitaftie chakula na kisha atapewa chakula na mfugaji.Pia kuku hawa huweza kufugwa huriaa yaani akaachwa kujitaftia chakula chake.



picha hapo juu ni vifaranga wa wiki moja baada ya kulishwa chick starter.

Friday 11 March 2016

Magonjwa ya kuku kwa ujumla yapo mengi sana na kuna baadhi ya magonjwa ambayo hayapo hapa nchini,ni vyema kujua dalili hizi za magonjwa mapema ili kuepusha hasara inayoweza kutokea kutokana na vifo ambavyo huchangiwa na magonjwa haya.
 Dalili hizo kwa ujumla ni kama ifuatavyo

1.   
     Kuku kupoteza hamu ya kula
2.        Kuku kuzubaa na kukaa sehemu moja kwa muda mrefu
3.        Kushuka kwa kiwango cha utagaji

4.        Vifaranga kudumaa
5.        Macho kua mekundu
6.        Kujikunja shingo
7.        Kutetemeka,kutoa maji maji puani,mdomoni na machoni
8.        Kutoa kinyesi chenye rangi ya kijani,au kinyesi kilicho changanyika na damu au cheupe.
9.        Kukohoa
10.     Kukonda

Endapo kuku wako ataonesha mojawapo ya dalili hizo basi mfugaji itamlazimu kutafta daktari wa mifugo au  kuku wapatiwe dawa.kujua madawa mbali mbali ya tazama post nyingine katika blog hii.Pia unaweza kufatilia mambo mbalimbali kuhusu kuku kupitia ukurasa wetu wa INSTAGRAM kwa jina la kukutajiri.

Saturday 27 February 2016

NENO LA USHAWISHI.......JE WEWE NI KIJANA NA UNAPENDA UFUGAJII???somaa hapaa

habari wasomaje na wafuatiliaji wa blog yetu,Leo ningependa kutoa neno la ushawishi kwa vijana wenzangu waliopo shuleni,vyuoni na mtaanii..je ni vipi unatumia muda wako baada ya masomo au kazi???umewahi kupata wazo la biashara??kama umewahi kupata wazo la biashara au la kukuingizia kipato ni kwanini hujaanza mpaka wakati huu???...MAWAZOO.......MAWAZOOO...Mawazo ni mazuri lakini yakifanyiwa kazi,mawazo yasipo fanyiwa kazi hakika kijana mwenzangu utabaki kuvusha tuu na kutamania maisha ya watu wengine.SIRI,siri ya mafanikio yoyote ni kufanya kazi,usiogope mtu mwenyewe mawazo makubwa,ila mheshimu sana mtu anaefanyia kazi mawazo yake.Hivyo siri ni moja,KUFANYA KAZI NA KUJITUMA KATIKA KILA JAMBO UFANYALO.


HII NI RATIBA YA CHANJO NA DAWA
1.     SIKU 1.
 Baada ya vifaranga kutotoreshwa wenye siku moja,vifranga wapewe glucose kwa muda wa masaa 2.Glucose huchanganywa katika maji na kupewa vifaranga hawa.baada ya hapo vifaranga wapewe vitamin mfano ni CHAMPRIX.Pia hii huchanganywa na maji.vifaranga wawe katika eneo lenye joto na safi. Baada ya hapo siku ya pili na kuendelea vifanga wapewe OTC plus(kijiko kimoja cha chai katika lita 5 za maji safi,pia changanya vitamin.


2.       SIKU YA 7.
vifaranga wapatiwe chanjo ya NEWCASTLE (KIDELI).chanjo hii huchanganywa na maji safi katika eneo lenye kivuli kasha kupewa vifaranga kwa muda wa masaa mawili kisha toa maji hayo na kuyamwaga mbali na eneo ambalo kuku wengine wanaweza kuyafikia,au kuyachimbia.baada ya hapo vifaranga wapewe maji yenye vitamin

mfano wa vifaranga wenye wiki moja(siku saba).Hawa wamepata chanjo ya newcastle na kama utakavyoona katika video hapa chini vifaranga wamechangamka.



3.     SIKU YA 14.
Wapewe chanjo ya GUMBORO(IBD).chanjo hii pia huchanganywa katika maji na kupewe vifaranga kwa muda wa masaa mawili tu.baada ya hapo vifaranga wepewe vitamin.



4.     Siku ya 21.(wiki ya tatu)
Rudia chanjo ya Newcastle



5.     SIKU 28(mwezi)
Rudia chanjo ya GUMBORO IBD


6.     SIKU 35(mwezi 1 na wiki 1)
Kipindi hiki kuku wapewe vitamin ya kutosha.


7.     WIKI YA 6-8
KUKU wapatiwe kinga ya ndui (fowl pox).kinga hii sio rahisi kwa mfugaji asie na utaalam kuwapa kuku,tafta mtaalum kwa kazi hii au upate maeleze ya jinsi ya kuweka kinga hii.
8.    WIKI YA 8
Kuku wapatiwe dawa ya minyoo na baada ya hapo unaweza kurudia chanjo ya Newcastle



Sample Text

Powered by Blogger.

Pages

watembeleaji wa mtandao wetu

Popular Posts

kukutajiri on facebook

fuatilia makala zetu kupitia facebook kupitia ukurasa wetu wenye jina la hapo juu
//]]>