Tuesday 1 November 2016

Habari za wakati huu wapenzi wasomaji wetu,Leo ningependa kutoa mawazo yangu kuhusu suala la kilimo nchini.
Tanzania ni nchi maskini,uchumi wa nchi hii unategemea zaidi kilimo.Kilimo huchangia asilimia 50 ya pato la ndani la nchi hii.Kumekua na jitihada mbalimbali za kuendeleza sekta hii ya kilimo nchini ikiwemo sera iliyo sikika sana ya "KILIMO KWANZA" .Jitihadi hizi zimeweza kufanikiwa kwa kiasi fulani ila kwa kiasi fulani bado uzalishaji wa malighafi nchi bado ni mdogo.
Baada ya kuhudhuria semina mbalimbali nilishangazwa kusikia hadi kuku tunaagiza kutoka nchi za jirani kama Malawi na Kenya.Ni aibu kubwa kwa taifa kama hili lenye ardhi kubwa na rasilimali watu.


VIFARANGA ZAIDI YA 5000 WALIOKAMATWA AIRPORT WAKIINGIZWA NCHINI KWA NJIA HARAMU

Nadhani ni wakati serikali ijaribu kutumia vijana wahitimu katika vyuo mbali mbali katika kuendeleza suala la kilimo nchini. Sera ya  KILIMO KWANZA ilikua na nia nzuri lakini imeonekana kama ilikua na nguvu ya soda,na pia ingelenga vijana moja moja ili kupunguza tatizo la ajira.
Pia vijana waelimishwe kuhusu kilimo,ufugaji na uvuvi ili waweze kujiajiri katika sekta hiyo.Nadhani iwepo sera kwaajili ya kuwahimiza vijana kuhusu kilimo na pia wapewe elimu na mikopo ili waweze kuingia katika uzalishaji malighafi kwa sababu tanzania ya viwanda inakuja hivyo vijana tuwe na Tanzania ya KILIMO ili tuweze kwenda sawa na kasi ya ukuaji wa teknolojia katika viwanda kwani viwanda vitahitaji malighafi hivyo si vyema kuagiza malighafi hizo nje ya nchini wakati nchi ina nguvu kazi na ardhi ya kutosha. Vijana turudi mashambani Tanzania ya tuijenge.

"VIJANA NA TANZANIA YA KILIMO"

KILIMO CHA CHIKICHI NA UTAJIRI KWA MKULIMA

KILIMO CHA UFUTA

UFUGAJI KUKU WA KIENYEJI NA MASOKO YAKE

Sample Text

Powered by Blogger.

Pages

watembeleaji wa mtandao wetu

Popular Posts

kukutajiri on facebook

fuatilia makala zetu kupitia facebook kupitia ukurasa wetu wenye jina la hapo juu
//]]>