Sunday 27 August 2017

Habari za wakati huu wasoma na wafuatiliaje wa mtandao wetu unaolenga katika kuelimisha watu hasa vijana katika ufugaji wa kuku wa kienyeji na chotara,Hivi karibuni watu wengi wamekua wakilalamika juu ya utotoleshaji mbovu wengi wamekua wikidhani ni mashine za kutotolesha,lakini tatizo kubwa ni sisi wafugaji kushindwa kutunza mayai vizuri,Hapa chini ni maelezo ya namna bora ya kutunza mayai kwaajili ya kutotolesha.



MAMBO MUHIMU KWA  YAI KUWEZA KUTOTOLESHWA
·        

       Yai lisizidi siku 7 mpaka 8 tangu litagwe

·        






Mayai yahifadhiwe kwenye trei yakitoka kuokotwa bandani

·         Zingatia Uwiano mzuri wa majogoo kwa matetea (1:8-10)

·         Mayai ya mtago wa kwanza sio mazuri kwa kutotolesha

·         Mayai ya kuku mzee sio mazuri kwa kutotolesha

·         Kuku watagaji wanapaswa kupewa chakula bora na cha kutosha

·         Mayai yahifadhiwe sehemu isio na joto kali

·         Mayai machafu hayafai kwa kutotolesha

·         Mayai madogo sana hayafai kwa kutotolesha

·         Mayai yenye kreki(nyufa)hayafai kwa kutotolesha

·         Mayai yenye umbo kubwa sana hayafai kwa kutotolesha

·         Mayai yenye viini viwili hayafai kwa kutotolesha

·         Yai lisihifadhiwe kwenye friji(hifadhi sehemu yenye hewa ya kutosha na isio na joto)

·         Wakati unahifadhi mayai katika trei hakikisha sehemu ya yai iliyochongoka inaangalia chini


·         Tengeneza viota kwaajili ya kuku kutagia ili kuepusha mayai yalio machafu.






KWA MAWASILIANO TUPIGIE KWA NUMBER ZIFUATAZO
0719342444/0788337971

0718616834

0 comments:

Post a Comment

Sample Text

Powered by Blogger.

Pages

watembeleaji wa mtandao wetu

Popular Posts

kukutajiri on facebook

fuatilia makala zetu kupitia facebook kupitia ukurasa wetu wenye jina la hapo juu
//]]>