Wednesday 2 September 2015


Habari za wakati huu wafuatiliaje wa machapisho yetu.Leo tutatazamia njia kuu mbili za kutotoresha mayai ya kuku wa kienyeji,njia hizo ni kumuacha kuku kutotoa mwenyewe na kumuwekea mazingira.njia ya pili ni kwa kutumia mashine za kutotoreshea.


NJIA ASILIA
kwa kutumia njia hii kuku ataachwa kutaga,kuatamia,na kutotoa mwenywe.mfugaji aandae mabox au mfuko kisha aweke vitu vyenye kutunza joto kama mchanga au matambaa kisha mabox hayo yawekwe katika mabanda ya kuku sehemu tulivu na yenywe kivuli


kuku hugata mayai 10-14 kutegemeana na aina ya kuku.kuku huweza kutotoa mayai 8-14


NJIA YA KISASA
Baada ya kuandaa sehemu ya kuku kutagia,kusanya mayai kila siku na kuweka katika trei.Uwekaji wa mayai hayo,sehemu kubwa ya yai iwe juu na incha yake iangalie chini.Hii husaidia katika utotoleshaji kwenye mashine.mashine hutotoresha vizuri zaidi endapo mayai yatakua yalikusanywa katika kipindi kifupi kuanzia siku 1-6 na kuwekwa katika mashine (incubator)

 MASHINE YA KUTOTORESHEA VIFARANGA(INCUBATOR)
Hii ni mashine ambayo hufanya kazi ya kuatamia na kutotoa mayai.mashine ina uwezo wa kutoto mayai mengi,mashine ndogo huweza kutotoa mayai 25-50.mashine hii hutoa joto sawa na joto la tetea,inashauliwa kugeuza geuza mayai kwa siku angalau mara tatu katika mashine ili kupata mazao bora zaidi.


CHANGAMOTO YA MASHINE HII
Inahitaji utaalamu kuitumia
inahitaji muda mwingi kukaa nayo karibu
ni gharama kuiendesha.

0 comments:

Post a Comment

Sample Text

Powered by Blogger.

Pages

watembeleaji wa mtandao wetu

Popular Posts

kukutajiri on facebook

fuatilia makala zetu kupitia facebook kupitia ukurasa wetu wenye jina la hapo juu
//]]>