Monday, 27 February 2017

Habari wapenzi wasomaji wetu,Leo napenda kuwaletea biashara ya vifaranga wa kuku chotara.Vifaranga wa mwezi mmoja wakiwa na chanjo kama
1.NEWCASTLE
2.GUMBORO
3. NDUI,

Pia wanunuzi wa vifaranga watapewa semina fupi kabla ya kupewa vifaranga.



Picha ya hapa chini ni baadhi ya vifaranga chotara wakina na mwezi mmoja.


Picha ya hapa chini ni vifaranga wa siku moja




Vifaranga hapa chini ni vifaranga wa wiki moja


 Wafugaji kutoka KUKUTAJIRI katika kazi ya ukusanyaji mayai kwaajili ya kwenda kutotolesha,je unajua sifa ya mayai bora kwaajili ya kutotolesha?endelea kufuatilia mtandao wetu utajifunza sifa hizo.

hapa chini ni kuku walezi kwaajili ya utagaji mayai ili yakatotoleshwe 

hapa chini ni aina ya jogoo kutoka kukutajiri.


kuku wazazi wakipewa chakula na wafugaji kutoka kukutajiri

bei ya vifaranga ni;
VIFANGA WA MWEZI NI TSH 4000/=
VIFARANGA WA SIKU NI TSH 2000/=
wasiliana nasi kwa namba 0719342444 au 0718616834

Tuesday, 1 November 2016

Habari za wakati huu wapenzi wasomaji wetu,Leo ningependa kutoa mawazo yangu kuhusu suala la kilimo nchini.
Tanzania ni nchi maskini,uchumi wa nchi hii unategemea zaidi kilimo.Kilimo huchangia asilimia 50 ya pato la ndani la nchi hii.Kumekua na jitihada mbalimbali za kuendeleza sekta hii ya kilimo nchini ikiwemo sera iliyo sikika sana ya "KILIMO KWANZA" .Jitihadi hizi zimeweza kufanikiwa kwa kiasi fulani ila kwa kiasi fulani bado uzalishaji wa malighafi nchi bado ni mdogo.
Baada ya kuhudhuria semina mbalimbali nilishangazwa kusikia hadi kuku tunaagiza kutoka nchi za jirani kama Malawi na Kenya.Ni aibu kubwa kwa taifa kama hili lenye ardhi kubwa na rasilimali watu.


VIFARANGA ZAIDI YA 5000 WALIOKAMATWA AIRPORT WAKIINGIZWA NCHINI KWA NJIA HARAMU

Nadhani ni wakati serikali ijaribu kutumia vijana wahitimu katika vyuo mbali mbali katika kuendeleza suala la kilimo nchini. Sera ya  KILIMO KWANZA ilikua na nia nzuri lakini imeonekana kama ilikua na nguvu ya soda,na pia ingelenga vijana moja moja ili kupunguza tatizo la ajira.
Pia vijana waelimishwe kuhusu kilimo,ufugaji na uvuvi ili waweze kujiajiri katika sekta hiyo.Nadhani iwepo sera kwaajili ya kuwahimiza vijana kuhusu kilimo na pia wapewe elimu na mikopo ili waweze kuingia katika uzalishaji malighafi kwa sababu tanzania ya viwanda inakuja hivyo vijana tuwe na Tanzania ya KILIMO ili tuweze kwenda sawa na kasi ya ukuaji wa teknolojia katika viwanda kwani viwanda vitahitaji malighafi hivyo si vyema kuagiza malighafi hizo nje ya nchini wakati nchi ina nguvu kazi na ardhi ya kutosha. Vijana turudi mashambani Tanzania ya tuijenge.

"VIJANA NA TANZANIA YA KILIMO"

KILIMO CHA CHIKICHI NA UTAJIRI KWA MKULIMA

KILIMO CHA UFUTA

UFUGAJI KUKU WA KIENYEJI NA MASOKO YAKE

Thursday, 27 October 2016

Habari za wakati huu wapendwa wasomaji wetu na wafugaji,leo ningependa kuwaalika kujifunza kitu kidogo kuhusu kuku chotara na tofauti yake na kuku 100% asilia.
 Kuku chotara hutaga mayai mengi zaidi kulinganisha na kuku 100% asili.kuku chotara hutaga mayai 220-280 kwa mwaka kulingana na ubora wa chakula na mfumo mzima wa ufugaji.



Tetea wa chotara hula kiasi cha 6.8kg kwa muda wa miezi mitano na kuweza kufikia uzito wa 1.8kg kwa kipindi hicho.

Jogoo chotara huweza hula kiasi cha 6.8kg kwa muda wa miezi mitano na kuweza kufikia uzito wa 2.6 kwa muda huo.

Matetea chotara huanza kutaga ndani ya muda wa miezi mitano mpaka sita kutegemea na utunzaji na vyakula wanavyopewe.

Ili kuku hawa watage sana wanatakiwa kula angalau 122g kwa siku za chakula kizuri ili kuweza kutaga kwa muda mrefu.
Kuku hawa wataanza tabia ya kudonoana kama wasipopewa chakula kizuri na chenye virutubisho vya kutosha pamoja na madini.Kuku hawa hudonoana sana na wakati mwingine hupelekea vifo na vidonda


Wednesday, 26 October 2016

Magonjwa ya kuku kwa ujumla yapo mengi sana na kuna baadhi ya magonjwa ambayo hayapo hapa nchini,ni vyema kujua dalili hizi za magonjwa mapema ili kuepusha hasara inayoweza kutokea kutokana na vifo ambavyo huchangiwa na magonjwa haya.
Dalili hizo kwa ujumla ni kama ifuatavyo
1.Kuku kupoteza hamu ya kula

2.Kuku kuzubaa na kukaa sehemu moja kwa muda mrefu
3.Kushuka kwa kiwango cha utagaji
4.Vifaranga kudumaa
5.Macho kua mekundu
6.Kujikunja shingo
7.Kutetemeka,kutoa maji maji puani,mdomoni na machoni
      8.Kutoa kinyesi chenye rangi ya kijani,au kinyesi kilicho changanyika na damu au cheupe.
9.  Kukohoa
10.  Kukonda sana

Endapo kuku wako ataonesha mojawapo ya dalili hizo basi mfugaji itamlazimu kutafta daktari wa mifugo au  kuku wapatiwe dawa.kujua madawa mbali mbali ya tazama post nyingine katika blog hii.Pia unaweza kufatilia mambo mbalimbali kuhusu kuku kupitia ukurasa wetu wa INSTAGRAM kwa jina la kukutajiri.

Kuku chotara/kienyeji hufungwa kwa matumizi ya kutaga mayai na pia kwa nyama.Mfugaji atachagua aina na mfumo wa chakula kutokana na yeye anafuga kuku hawa kwa matumizi gani.

Ili kuku wafugwe kwaajili ya mayai fuata ratiba hii ya chakula

Chick starter kwa muda wa miezi miwili(2)
Grower Mash kwa muda wa miezi miwili na nusu(2.5)
Layers mwezi mmoja na kuendelea.

Ili kuku wafugwe kwaajili ya nyama fuata ratiba hii ya chakula

Broiler starter-mwezi mmoja(1)
Grower Mash-Mwezi mmoja(1) 
Broiler Finisher-Mwezi mmoja(1)


Ili kuku wafugwe na kutaga mayai kwaajili kutotolesha fuata ratiba hii ya chakula

Chick Starter-miezi miwili(2)
Grower mash-miezi miwili na nusu(2.5)
Breeders mash-mwezi mmoja na kuendelea.hakikisha majogoo wanapunguzwa na kubaki na uwiano wa jogoo mmoja kwa matetea kumi(1:10)







Ratiba hii ni kwa ufugaji wa kibiashara lakin mfugaji anaweza kuwafuga kuku hawa kwa mfumo wa nusu huria yaani kuku akaachiwa ajitaftie chakula na kisha atapewa chakula na mfugaji.Pia kuku hawa huweza kufugwa huriaa yaani akaachwa kujitaftia chakula chake.



picha hapo juu ni vifaranga wa wiki moja baada ya kulishwa chick starter.

Friday, 11 March 2016

Magonjwa ya kuku kwa ujumla yapo mengi sana na kuna baadhi ya magonjwa ambayo hayapo hapa nchini,ni vyema kujua dalili hizi za magonjwa mapema ili kuepusha hasara inayoweza kutokea kutokana na vifo ambavyo huchangiwa na magonjwa haya.
 Dalili hizo kwa ujumla ni kama ifuatavyo

1.   
     Kuku kupoteza hamu ya kula
2.        Kuku kuzubaa na kukaa sehemu moja kwa muda mrefu
3.        Kushuka kwa kiwango cha utagaji

4.        Vifaranga kudumaa
5.        Macho kua mekundu
6.        Kujikunja shingo
7.        Kutetemeka,kutoa maji maji puani,mdomoni na machoni
8.        Kutoa kinyesi chenye rangi ya kijani,au kinyesi kilicho changanyika na damu au cheupe.
9.        Kukohoa
10.     Kukonda

Endapo kuku wako ataonesha mojawapo ya dalili hizo basi mfugaji itamlazimu kutafta daktari wa mifugo au  kuku wapatiwe dawa.kujua madawa mbali mbali ya tazama post nyingine katika blog hii.Pia unaweza kufatilia mambo mbalimbali kuhusu kuku kupitia ukurasa wetu wa INSTAGRAM kwa jina la kukutajiri.

Saturday, 27 February 2016

NENO LA USHAWISHI.......JE WEWE NI KIJANA NA UNAPENDA UFUGAJII???somaa hapaa

habari wasomaje na wafuatiliaji wa blog yetu,Leo ningependa kutoa neno la ushawishi kwa vijana wenzangu waliopo shuleni,vyuoni na mtaanii..je ni vipi unatumia muda wako baada ya masomo au kazi???umewahi kupata wazo la biashara??kama umewahi kupata wazo la biashara au la kukuingizia kipato ni kwanini hujaanza mpaka wakati huu???...MAWAZOO.......MAWAZOOO...Mawazo ni mazuri lakini yakifanyiwa kazi,mawazo yasipo fanyiwa kazi hakika kijana mwenzangu utabaki kuvusha tuu na kutamania maisha ya watu wengine.SIRI,siri ya mafanikio yoyote ni kufanya kazi,usiogope mtu mwenyewe mawazo makubwa,ila mheshimu sana mtu anaefanyia kazi mawazo yake.Hivyo siri ni moja,KUFANYA KAZI NA KUJITUMA KATIKA KILA JAMBO UFANYALO.


Sample Text

Powered by Blogger.

Pages

watembeleaji wa mtandao wetu

Popular Posts

kukutajiri on facebook

fuatilia makala zetu kupitia facebook kupitia ukurasa wetu wenye jina la hapo juu
//]]>