Tuesday 18 August 2015

 


   habari za wakati huu wasomaji na wafuatiliaji wa blog yetu.leo ningependa kuchambua faida mbalimbali za kuku wa kienyeji.Imezoeleka katika sehemu nyingi kuku hutumika kama kitoweo,hii ni faida moja wapo ya kuku,lakini pia mayai ya kuku wa asili hua na virutubisho kama Vitamin A,Vitamin E,Vitamin D,vitamin B12,madini ya zinc,madini chuma na pia protein ambayo ni muhimu sana katika ujenzi wa mwili.                                                                                  

   kuku hufugwa kiabishara ni ajira nzuri kwa mfugaji.ufungaji wa kuku huitaji mtaji kidogo katika kuanzisha,pia eneo la dogo.mfano unaweza kuanza na mtaji wa kuku 7,matetea watano na majogoo watatu.kama kuku hawa watapata chakula kilicho bora kuku mmoja huweza kutaga na kutoto hadi vifaranga 12.hivyo kwa matetea watano huweza kufikisha hadi vifaranga 50.mfugaji akiweza kulea Angalau vifaranga 40  ukijumlisha na wale Saba wa mwanzo ni jumla ya kuku 47.kwa idadi hiyo ya kuku inamaana kutakua na ongezeko kubwa la utotoleshaji.kwa wafugaji wasio kua na mtaji mkubwa unaweza kuuza kuku hata kumi kwa bei ya kuanzia 20000/= hadi 25000/=  ambapo huweza kupata laki 2 (200,000/=).fedha hii ikatumika katika kununua chakula na madawa kupambana na magonjwa.kwa njia huu mfugaji huweza hata kufikia kuku 1000 hivyo kufanya mfungaji
kua na mtaji wa 20,000,000.kwa wasio na maeneo ya kutosha ,usiogope biashara hii hujiendesha yenyewe ukianza vizuri unaweza kuuza mayai au kiasi fulani cha kuku ,fedha hiyo ikatumika katika kujiendeleza katika biashara hii.
kuku huliwa kila siku sehemu mbali mbali kama kwenye migahawa,hotelini na kwa mama ntilie hivyo solo lake in la uhakika.
Mali ghafi za kujengea bandana ya kuku hupatikana kirahisi katika sehemu mbali mbali  hata maeneo ya vijijini.Pia vifaa vyake hupatikana katika maduka ya mifugo na huweza kujengwa vifaa vya asili katika maeneo  yasio na maduka hayo.

usikose kutembelea blog hii kwa taarifa nyingine zaidi kuhusu ufugaji wa kuku

0 comments:

Post a Comment

Sample Text

Powered by Blogger.

Pages

watembeleaji wa mtandao wetu

Popular Posts

kukutajiri on facebook

fuatilia makala zetu kupitia facebook kupitia ukurasa wetu wenye jina la hapo juu
//]]>