Wednesday 27 September 2017

Mapungufu ya Kuku wa Asili:
Hutaga mayai madogo wastani wa gramu 47 ambapo kuku wa kisasa wastani wa gramu 55,aidha hutaga mayai machache wastani wa mayai 60 kwa mwaka ambapo kuku wa kisasa huweza kutaga hadi mayai 300 kwa mwaka.(CHOTARA NA KROILERS HUTAGA MAYAI 240-260 KWA MWAKA)
Ukuaji taratibu – kuku wa asili hukua taratibu kutokana na lishe duni. Kutokana na hali hiyo kuku
huchukua muda mrefu (miezi sita) kufikia uzito wa kuchinjwa (kilo 1 - 1.5). Hali hii pia hufanya faida ya ufugaji wa kuku wa asili kuchukua muda mrefu kupatikana.
Nyama yake ni ngumu (huchukua muda mrefu kuiva) ikilinganishwa na kuku wa kisasa.

Changamoto katika ufugaji kuku wa asili:
1. Mabanda: Ukosefu wa mabanda bora.
2. Wezi, wanyama na ndege hushambulia kuku.
3. Magonjwa: kama mdondo na ndui huathiri ufugaji wa kuku.
4. Tabia na miiko ya baadhi ya jamii. Baadhi ya jamii za makabila hapa nchini huona ufugaji wa kuku kama ni kitu duni.
5. Upatikanaji haba wa chanjo za magonjwa kama vile, mdondo, ndui, homa ya matumbo.

6. Si rahisi kuweza kupata kabila halisi (Pure breed) au kizazi halisi (Pure line) za kuku wa Asili
7. kutokana na mazingira ya muingiliano wa vizazi kati ya aina mbalimbali za kuku hao. Hata hivyo
8. kuku hawa wana tofauti za kimaumbile zilizosababisha kuwepo kwa kabila mbalimbali baina yao.
9. Kabila hizi pia zinahusishwa kwa kiasi kikubwa na eneo kuku hao wanakotoka.
10. Kutokana na muingiliano wa vizazi, maumbile hayo yanaweza yakajitokeza kwenye aina mbalimbali za kuku, ikiwa na maana kwamba kuku mmoja kuwa na kabila moja au zaidi kwa mara moja. Hivyo aina za kuku zifuatazo zinaweza kutambuliwa kama ndiyo kabila za kuku wa Asili kulingana na maumbile yao na maeneo wanakotoka.

0 comments:

Post a Comment

Sample Text

Powered by Blogger.

Pages

watembeleaji wa mtandao wetu

Popular Posts

kukutajiri on facebook

fuatilia makala zetu kupitia facebook kupitia ukurasa wetu wenye jina la hapo juu
//]]>